• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Frequently Asked Questions |
Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe

The United Republic of Tanzania MBOGWE DISTRICT COUNCIL MBOGWE DISTRICT COUNCIL

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Administration and human resource
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Finance and Business
      • Social Work
      • Health
      • Ardhi na Mali Asili
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji na Udhibiti Majitaka
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Units
      • Procurement and Supply
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa na Uwekezaji
  • Huduma
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Hamashauri ya Mbogwe
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu,Afya Na Maji
      • Kamati ya Maaadili
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Bodi ya Ajira
      • Alat Mkoa
      • Kamati ya Vileo
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi(CMAC)
      • Kamati ya Kugawa Ardhi
      • Kamati ya LAVULAK
  • Miradi
    • Project Projection
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha za Matukio mbalimbali
  • Machapisho
    • Bajeti na Taarifa za Mapato
    • Fomu mbalimbali

Madiwani Wametakiwa Kuwahimiza Wananchi Walioko Kwenye Mpango wa TASAF Kuunda Vikundi

Posted on: May 8th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Mbogwe Mhe. Martha Mkupasi amewataka madiwani wenye vijiji vyenye walengwa wa mpango wa TASAF awamu ya tatu kuwaelimisha wanufaika wa mpango huo wa kunusuru kaya maskini kuhusu umuhimu wa kuweka akiba na kukuza uchumi wa kipato cha kaya.

Mkuu wa wilaya ameyasema hayo wakati wa kufungua kikao kazi cha waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Idara pamoja na Maafisa Ugani wa wilaya ya Mbogwe kilichofanyika leo tarehe 8-5-2018 katika ukumbi waHalmashauri.

Kikao hicho kimeendeshwa na wataalam kutoka TASAF makao makuu pamoja na Wataalam kutoka Halmashauri za wilaya ya Ikungi na Mbogwe, kikiwa na lengo la kuwajengea uwezo waheshimiwa Madiwani ,Wakuu wa idara na Maafisa ugani ili wawe na uelewa sahihi kuhusu uwekaji wa akiba na ukuzaji wa uchumi wa kaya.

Mpango wa TASAF awamu ya tatu umeanza rasmi Wilayani hapa ukiwa unatekeleza  kipengele cha tatu cha kuondoa umaskini wa kaya kiitwacho "Kuweka akiba na kukuza uchumi wa kipato cha kaya""

Ambapo kipengele cha kwanza na cha pili yaani uhawilishaji fedha na miradi inayotoa  ajira za muda vitaendelea sambasamba na kipengele hiki kipya cha tatu kinachoanza rasmi kupitia fedha wanazopata katika uhawilishaji na pia kazi wafanyazo katika miradi ya ajira za muda, wataweza kuweka akiba ili kuinua kipato cha kaya.

Pamoja na hayo muwezeshaji wa mafunzo toka TASAF makao makuu ndugu Sesil Charles Latemba amewaomba Waheshimiwa Madiwani kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelimisha wananchi kuhusu utunzaji wa akiba,

Vile vile amewasisitizia wazingatie kuwa uundwaji wa vikundi vya kujiwekea akiba ni swala la hiari hivyo wajikite katika kuwaelimisha umuhimu wa kuwa kwenye vikundi.

Pia Bwana Latemba amewaambia Madiwani wakati akijibu swali la mmoja wa washiriki kwamba vijiji ambavyo havikuingizwa kwenye mpango, jitihada za Serikali, wadau wa maendeleo na TASAF bado zinaendelea ili hatimaye Vijiji hivyo  viingizwe kwenye mpango,  kwa sasa wasiwaahaidi wananchi chochote mpaka hapo itakavyoelekezwa rasmi kufanya hivyo.

Akiongea kwa niaba ya Madiwani, Diwani wa Kata ya Ilolangulu Mhe. Ndabacha Simon ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali wananchi maskini, pia kuanza mchakato wa kuviongeza vijiji ambavyo havikuwa kwenye mpango wa TASAF.



Announcements

  • Watoto wa kike waliokatisha Masomo yao November 01, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA USAJILI WA ANWANI ZA MAKAZI March 09, 2022
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi kwa Walimu September 06, 2020
  • Ratiba ya Kampeni za Kampeni Jimbo la Mbogwe August 26, 2020
  • View All

Latest News

  • WAENDESHA VIFAA VYA BIOMETRIKI NA WAANDISHI WASAIDIZI WAKIPATA MAFUNZO

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA WAENDESHA VIFAA VYA BIOMETRIKI NA MAFUNZO YA WAANDISHI WASAIDIZI YAMEFANYIKA LEO TAREHE 29 APRILI,2025

    April 29, 2025
  • TAARIFA YA MKAGUZI WA MAHESABU

    June 26, 2024
  • Progamu ya utoaji wa Chakula Mashuleni wilayani Mbogwe

    May 20, 2022
  • View All

Video

UFUNGUZI WA MAJENGO MAPYA NA UPANUZI WA KITUO CHA AFYA CHA MASUMBWE, GEITA
More Videos

Quick Links

  • MKOA WA GEITA
  • WIZARA YA TAMISEMI
  • IKULU YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
  • MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA(TRA)
  • BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA(NECTA)
  • WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
  • WIZARA YA ELIMU,SAYANSI NA TKNOLOJIA
  • WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Related Links

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora
  • Mkoa wa Geita

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

    Mbogwe District council ,Masumbwe-Mbogwe,Geita

    Postal Address: P.O Box 1 Masumbwe

    Telephone: +255734412592

    Mobile: +255734412592

    Email: ded@mbogwedc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.