• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Frequently Asked Questions |
Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe

The United Republic of Tanzania MBOGWE DISTRICT COUNCIL MBOGWE DISTRICT COUNCIL

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Administration and human resource
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Finance and Business
      • Social Work
      • Health
      • Ardhi na Mali Asili
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji na Udhibiti Majitaka
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Units
      • Procurement and Supply
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa na Uwekezaji
  • Huduma
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na mazingira
      • Kamati ya Elimu Afya na Maji
  • Miradi
    • Project Projection
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha za Matukio mbalimbali
  • Machapisho
    • Bajeti na Taarifa za Mapato
    • Fomu mbalimbali

Bee Unit

Mkuu wa Kitengo

Imelda Gwassa

A: UTANGULIZI:

Kitengo cha Ufugaji nyuki kilianzishwa rasmi Februari, 2016 kikiwa na malengo ya kuongeza uzalishaji na ubora wa mazao ya nyuki pamoja na kukuza kipato cha wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla wake. Kwa kutambua umuhimu huu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe imeendelea kuhamasisha ufugaji wa nyuki kupitia vikundi na watu binafsi katika kata za Iponya, Masumbwe, Nyakafuru, Bukandwe, Nhomolwa, Lugunga, Mbogwe, Nanda na Ngemo. Takribani watu 410 wanajishughulisha na ufugaji wa nyuki

B:HUDUMA ZITOLEWAZO NA KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI:

Ili kukuza na kuendeleza ufugaji bora na wa kisasa wa nyuki, majukumu ya Kitengo hiki ni:

  1. Kuboresha huduma za ugani kwa kutoa elimu ya ufugaji bora wa nyuki kwa wakati

  2. Kuhamasisha na kuanzisha vikundi vya wafugaji nyuki katika Kata au Kijiji

  3. Kutoa elimu ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira ambayo nyuki watatumia kutengeneza asali

  4. Kuhakikisha njia za urinaji wa asali zinazotumika haziui nyuki wala kuharibu mazalia au masega yao

  5. Kusimamia ubora wa mazao ya nyuki ili kulinda afya ya mtumiaji

  6. Kutengeneza mizinga bora ya mfano kwa ajili ya ufugaji wa nyuki na kufundishia

  7. Kuwezesha upatikanaji rahisi wa zana na vifaa vya kisasa vya kuvunia asali

  8. Kuwatafutia wafugaji soko la uhakika la asali

  9. Kuwasaidia wakulima walioko katika vikundi kuanzisha vituo vya kukusanyia na kuuza asali

  10. Kuanzisha mashamba darasa ya ufugaji wa nyuki na hifadhi ya mazingira

  11. Kufanya tathmini ya kila mwaka ya ukuaji wa sekta ya ufugaji wa nyuki

  12. Kuwezesha vikundi vya wafugaji wa nyuki kuhudhuria maoneshoya siku ya wakulima nane nane ili kuonesha bidhaa zao katika kanda husika

  13. Kuwashawishi wananchi kuanzisha vyama vya kuweka na kukopa ili kukuza mitaji

  14. Kutenga maeneo maalum ya ardhi kwa ajili ya wafugaji wa nyuki

  15. Kutoa huduma bora kwa wadau wote kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma.

  16. Kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo za Hifadhi, Afya na Usafi wa Mazingira za Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe.

C: IKAMA YA WATUMISHI

Kitengo cha ufugaji nyuki kina mtumishi mmoja.

 D: TAKWIMU MUHIMU ZA KITENGO

Takwimu zinaonesha kwamba takribani watu 410 wanajishughulisha na ufugaji nyuki. Maeneo muhimu, idadi ya mizinga na vikundi ni kama inavyoonesha katika jedwali:

Na.
KATA
MIZINGA YA KISASA
MIZINGA YA KIENYEJI
JUMLA YA MIZINGA
JUMLA YA VIKUNDI
1
MASUMBWE
40
78
118
5
2
IPONYA
563
18,649
19,212
3
3
NYAKAFURU
2
77
79
2
4
NHOMOLWA
48
70
118
2
5
BUKANDWE
96
230
326
4
6
LUGUNGA
10
0
10
1
7
NANDA
10
207
217
1
8
NGEMO
22
41
63
0
9
MBOGWE
18
504
522
1

JUMLA
761
19,786
20,547
19

 

 E: WAJIBU WA MFUGA NYUKI

Wajibu wa mfuga nyuki ni:

  1. Kutumia mizinga ya kisasa katika ufugaji nyuki

  2. Kurina asali kwa kutumia njia za kisasa badala ya kutumia moshi au moto

  3. Kuhifadhi mazingira kwa kutochoma moto au misitu

  4. Kujiunga katika vikundi vya uhifadhi ya mazingira

  5. Kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa vya wafugaji wa nyuki

  6. Kutumia dawa isiyoua nyuki wala kuharibu ubora wa asali wakati wa urinaji

  7. Kutumia vyombo au vifaa vilivyo safi na salama kwa ajili ya kurinia na kuhifadhia asali

  8. Kuhudhuria mafunzo yatolewayo katika mashamba darasa ya ufugaji wa nyuki

F: MAKOSA KWA MJIBU WA SHERIA NDOGO ZA HALMASHAURI

Mdau yeyote atakuwa ametenda kosa endapo atafanya mambo yafuatayo:

  1. Atarina asali kwa kutumia moto au moshi

  2. Atauza asali iliyorinwa kwa moto au moshi

  3. Atachanganya au amechanganya asali na vitu vingine ambavyo siyo asali

  4. Atachoma moto msitu au eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya wafugaji wa nyuki

  5. Atakata miti bila kuwa na kibali kutoka Halmashauri

  6. Atang’oa miti iliyopandwa kwa ajili ya kuhifadhi mazinggira

  7. Atatenda jambo lolote ambalo linadhuru au linahatarisha maendeleo na ukuaji wa kilimo cha nyuki

  8. Atatenda kitendo chochote kinachohatarisha upatikanaji wa asali yenye ubora na salama

  9. Atahujumu miundo mbinu ya ufugaji wa nyuki ya shule, kikundi, kijiji, mtaa, kata, taasisi na mtu binafsi

Na akipatikana na hatia chini ya kifungu cha 26 cha sheria Ndogo za Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe, atatozwa faini isiyopungua elfu hamsini (50,000/=) na isiyozidi shilingi laki tatu (300,000/=) au kifungo kisichozidi miezi kumi na mbili jela au vyote viwili yaani kifungo na faini.

G:UWEKEZAJI

  1. Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe kwa kushirikiana na TFS walitoa jumla ya mizinga 330 ya kisasa aina ya kati kwa vikundi vya ufugaji nyuki katika kata za Iponya, Masumbwe, Nyakafuru, Nanda, Mbogwe, Lugunga, Nhomolwa, Bukandwe na Ngemo.

  2. Mafundi seremala 10 kutoka kata za Iponya, Mbogwe na Masumbwe walipatiwa mafunzo ya utengenezaji wa mizinga ya kisasa aina ya katiyaliyofanyika Mwanza Oktoba,2015.

H: CHANGAMOTO

Pamoja na mafanikio ya ufugaji nyuki pia zipo changamoto katika sekta hii.

  1. Shughuli za kibinadamu katika maeneo ya ufugaji nyuki kama ukataji miti ovyo kwa ajili ya mkaa, mbao, uchomaji matofali, ukaushaji wa tumbaku na matimba kwa ajili ya kuweka kwenye mashimo ya wachimbaji wadogo wadogo wa madini, utayarishaji wa mashamba kwa kukata miti na kuchoma moto na Ufugaji wa mifugo kwenye maeneo ya ufugaji nyuki.

  2. Uhaba wa maeneo binafisi ya ufugaji nyuki

  3. Upungufu wa Wataalam wa ufugaji nyuki

I: MIKAKATI YA KUENDELEZA SEKTA YA NYUKI

Mikakati madhubuti inahitajika ili kuendeleza sekta ya ufugaji nyuki katika utoaji wa huduma bora kwa jamii. Katika kukabiliana na changamoto zilizopo mikakati ifuatayo ni muhimu ikazingatiwa:

  1. Kuendelea kutoa elimu ya hifadhi bora ya mazingira kwa jamii na kufanya doria za mara kwa mara ili kubaini na kuzuia ukataji ovyo wa miti katika maeneo ya ufugaji nyuki

  2. Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa kuwawezesha wafugaji nyuki kuwa na hati miliki ya maeneo ya ufugaji

  3. Kuongeza wataalam wa sekta ya ufugaji nyuki ili kuboresha utoaji wa huduma bora kwa jamii


Announcements

  • Watoto wa kike waliokatisha Masomo yao November 01, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA USAJILI WA ANWANI ZA MAKAZI March 09, 2022
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi kwa Walimu September 06, 2020
  • Ratiba ya Kampeni za Kampeni Jimbo la Mbogwe August 26, 2020
  • View All

Latest News

  • Progamu ya utoaji wa Chakula Mashuleni wilayani Mbogwe

    May 20, 2022
  • Maadhimisho ya Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    April 26, 2022
  • Maadhimisho ya Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    April 26, 2022
  • Mkurugenzi Mtendaji Bi Saada Selemani Mwaruka katika Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

    April 26, 2022
  • View All

Video

UFUNGUZI WA MAJENGO MAPYA NA UPANUZI WA KITUO CHA AFYA CHA MASUMBWE, GEITA
More Videos

Quick Links

  • MKOA WA GEITA
  • WIZARA YA TAMISEMI
  • IKULU YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
  • MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA(TRA)
  • BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA(NECTA)
  • WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
  • WIZARA YA ELIMU,SAYANSI NA TKNOLOJIA
  • WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Related Links

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora
  • Mkoa wa Geita

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

    Mbogwe District council ,Masumbwe-Mbogwe,Geita

    Postal Address: P.O Box 1 Masumbwe

    Telephone: +255734412592

    Mobile: +255734412592

    Email: ded@mbogwedc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.