Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Adv. Edwin Lusa amewataka Maafisa Elimu Ngazi ya Halmashauri,Maafisa wa Tume ya Utumishi wa Walimu,Wathibiti Ubora wa Shule,Maafisa Elimu Kata,Viongozi wa Umoja wa Walimu Wakuu na walimu Wakuu kushirikiana kwa pamoja kuongeza kiwango cha Taaluma na Ubora wa Elimu Msingi kutoka Asilimia 74 hadi Asilimia 85 na zaidi kwa kupitia Usimamizi bora wa Ufundishaji ,Matumizi bora ya rasilimali,Matumizi ya Mbinu na Zana bora, Ufuatiliaji wa mara kwa mara na Ushirikishwaji kwa Jamii.
Adv. Lusa ametoa Agizo hilo Leo Januari 17,2026 katika kikao Kazi chake na Maafisa Elimu ngazi ya Halmashauri,Maafisa wa Tume ya Utumishi wa Walimu,wathibiti Ubora wa Shule ,Maafisa Elimu Kata ,Viongozi wa umoja wa Walimu na Walimu Wakuu kilichofanyika katika Shule ya Msingi Masumbwe Kata ya Masumbwe.
Amesema wanao wajibu wa kuongeza Wastani wa Ufaulu wa Wanafunzi ili kuboresha Matokeo ya kitaaluma ya Wanafunzi kupitia Ufundishaji wenye tija na Tathmini.
Aidha amewataka kupunguza Utoro wa Wanafunzi sambamba na kuboresha Nidhamu,Bidii na Uwajibikaji katika masomo kwa Wanafunzi kwa kujenga tabia chanya za Kitaaluma kwa Wanafunzi katika kujifunza.
Sambamba na hayo amewataka Walimu Wakuu kusimamia kikamilifu miradi mbalimbali ya Maendeleo ambayo inaendelea katika Shule zao kwa kuwabana mafundi pamoja na wazabuni ili iweze kukamilika kwa wakati.
Nae Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Elimu Awali na Msingi Zenaida Msita amesema Lengo kuu ni kuiinua kiufaulu Wilaya ya Mbogwe hivyo ipo haja kubwa ya viongozi hao kishirikiana katika kuongeza Wastani wa Ufaulu kwa Wanafunzi.
Mbogwe District council ,Masumbwe-Mbogwe,Geita
Postal Address: P.O Box 1 Masumbwe
Telephone: +255734412592
Mobile: +255734412592
Email: ded@mbogwedc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.