Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe imepongezwa kwa kupata Hati Safi kwa Miaka Mitatu Mfululizo kuanzia Mwaka 2021/2022 hadi Mwaka 2023/2024.
Pongezi hizo zimetolewa leo Tarehe 16 Juni, 2025 na Mhe. Sakina Mohamed Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe ambaye ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita katika Mkutano Maalum wa Baraza la kupokea na kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Shule ya Sekondari Masumbwe Kata ya Nyakafuru.
"Twendeni tukasimamie vizuri fedha za Miradi ya Maendeleo na tuhakikishe tunakabidhi nyaraka zote muhimu kwa Mkaguzi wa nje ili tuweze kufunga hoja zilizobaki na tuepuke kuongeza hoja nyingine " amesisitiza Sakina.
Kwa upande wake Mkaguzi Mkuu wa Mkoa wa Geita (Chief External Auditor) Bw. Waziri Shabani wakati akiwasilisha ripoti amesema Jumla ya Hoja mpya za mwaka wa ukaguzi (2023/ 2024) ni Hoja 23 ikiwa Hoja zilizofungwa ni 13 sawa na 56.5 % na kusalia Hoja 10. Katika Hoja Za miaka ya nyuma (kuishia 30, Juni 2023) zilikuwa hoja 38,na zimefungwa hoja 21 sawa na 55.3% na kusalia Hoja 17.
Matukio ya picha katika Baraza Maalumu la Kupokea na Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)
Matukio ya picha katika Baraza Maalumu la Kupokea na Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)
Matukio ya picha katika Baraza Maalumu la Kupokea na Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)
Matukio ya picha katika Baraza Maalumu la Kupokea na Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)
Mbogwe District council ,Masumbwe-Mbogwe,Geita
Postal Address: P.O Box 1 Masumbwe
Telephone: +255734412592
Mobile: +255734412592
Email: ded@mbogwedc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.